Wednesday, 15 February 2017

Je wewe ni mmoja wa Kanisa litakalonyakuliwa na Yesu

Hii ina maana gani?

Kitambo kidogo kinakuja ambapo kanisa la Mungu, wale waliompokea Yesu Kristo kuwa Bwana na Mwokozi wa maisha yao na kuishi maisha yanayoongozwa na Roho Mtakatifu katika kila eneo la maisha yao, watanyakuliwa kwa uweza wa Roho Mtakatifu kuelekea mawinguni kumlaki Bwana Yesu, pale panda itakapolia. Nao wataelekea mbinguni kwenye karamu ya Mwanakondoo, na Kanisa ndilo Bibi harusi. (1Wathesalonike 4:17, Matendo ya mitume1:11)

Kitu gani cha kufanya ili kuwa mmoja wa Kanisa la Bwana Yesu Kristo?

Mpokee Yesu Kristo ndani ya maisha yako na yeye awe Bwana na Mwokozi wako hivyo ulivyo. Yesu Kristo atakupokea na kukusafishana damu yake na kukuwezesha kuishi maisha ya mabadiliko ya kumpendeza yeye. (Warumi 3:23, Warumi 6:23, Warumi 5:8, Warumi 10:13, Warumi 10:11,Mathayo 10:32)

Kitu gani hutokea ukimpokea Kristo ndani ya moyo wako?

  • Unapata msamaha wa dhambi zako zote, jina lako linaandikwa katika kitabu cha Mungu.
  • Utampokea Roho Mtakatifu atakayekufundisha njia ya kumpendeza Mungu  na kukupa ushindi juu ya dhambi, tamaa za dunia na shetani.
  • Utaishi kwa matumaini bila woga
  • Utapata furaha ya ndani ya moyo na amani hata kama unapitia magumu
  • Utaanza kujua siri za Mungu kuhusu majira na nyakati muhimu zinazohusu watu wake yaani Kanisa na Israel.
  • Unakuwa katika hali yakuwa tayari kukutana naYesu ajapo kuchukua walio wake hapa duniani.
Kitu gani hutokea usipo mpokea Yesu Kristo ndani ya moyo wako?
  • Unaishi maisha ya woga na kukosa matumaini ya siku zijazo
  • Unaishi kwa kutegemea uweza wako na wa wengine
  • Unakuwa bize na mafanikio ya duniani
  • Hupendelei kusikiliza neno la Mungu
  • Unakuwa hauna taarifa ya namna ya kujitayarisha kwa ujio wa Bwana Yesu
  • Utaachwa duniani wakati kanisa linachukuliwa na Bwana Yesu kuelekea mbinguni
Kama utapenda kumpokea BwanaYesu ndani ya moyo wako, sali sala hii kwa kumaanisha.

Bwana Yesu, nakuja mbele zako kwa moyo wangu wote na kwa akili zangu zote. Naomba unisamehe dhambi zangu zote. Asante kwa kufa msalabani kwa ajili yangu. Nakupokea sasa ndani ya moyo wangu na maisha yangu. Damu yako ya thamani na initakase iniweke huru sasa mbali na dhambi. Niponye na magonjwa yote. Futa jina langu katika kitabu cha hukumu. Andika jina langu katika kitabu cha uzima cha mwanakondoo. Nijaze na Roho Mtakatifu anifundishe kukujua wewe. Naomba haya kwa jina la Yesu Kristo. Amen.

Kama umeomba sala hii kwa kumaanisha, umempokea Bwana Yesu ndani ya moyo wako. Umekuwa mmoja wa kanisa la Mungu hapa duniani. Omba uongozi wa Roho Mtakatifu kila siku. Pia unaweza kunijulisha kwa kunitumia barua pepe integritythewaytosuccess@gmail.com au nipigie kwenye 
255 782 880 330/ 255 758 764 539

1 comment: