Zaburi 107:19-20 inasema “Wakamlilia Bwana katika shida zao.
Akawaponya na shida zao.Hulituma neno lake huwaponya. Huwatoa katika maangamizi”
Ashukuriwe Mungu aliye juu kwakuwa tunalo tumaini katika
yeye. Kwakuwa ndiye ngome yetu na msaada wetu wakati wa mateso.
Leo ningependa nikukumbushe kwa habari ya kumlilia Mungu
katika shida uliyonayo.Kwa maana imeandikwa muite Mungu maadamu anapatikana.
Mara nyingi tunakuwa katika shida na taabu katika maisha
yetu na tunakaa hapo hapo katika hiyo shida kwa muda mrefu sana kuliko ilivyotakiwa. Ni
kwanini? Hii ni kwasababu hatumlilii Mungu katika shida zetu. Unaweza kujiuliza
mbona huwa ninaomba sana lakini majibu hayaji. Hii pia ni kwasababu unaomba
vibaya. Imeandikwa kuwa” hampati kwasababu mnaomba vibaya”.
Kuomba vibaya ni kwa namna gani?
Ni kwa kulalamika na kuliangalia tatizo lako zaidi ya kumuangalia
Mungu na uweza wake wa kuliondoa tatizo. Mara nyingi unakuwa na maombi
yanayotokana katika nafsi yako kuliko yanayotoka rohoni. Rohoni ni mahali
pasipo na waa na ndipo Mungu hukaa. Kwenye nafsi yako ni mahali unafanya
maamuzi kutokana na hali halisi inayokuzunguka. Hivyo kuomba vizuri ni kuomba
sawasawa na neno la Mungu, na si mapenzi yako.
Tukiweza kuomba sawasawa na neno lake, atasikia. Mara kwa
mara tunaomba sawasawa na mapenzi yetu, na ndipo Mungu hatusikiii kwasabau
hujaingia bado kwenye himaya yake. Kulia sana na uchungu sana hausaidii na tena
imeandikwa “uchungu wote na uondoke kwenu.”
Embu chunguza hayo unayomuomba Mungu na namna unavyomuomba,
je unaomba kwa hisia ya mwilini au katika roho? Mungu ni roho, ukitaka kuongea
nae uwe katika roho na ndipo Roho Mtakatifu hutusaidia pale tunaposhindwa
kuomba katika roho.
Nakusihi uanze kutafuta kujua namna ya kumuomba Mungu katika
roho na utaona jinsi majibu utakavyoyapata kwa haraka kama neno linavyosema
walimlilia, wakaponywa na kuondolewa katika maangamizi yao.
Mungu yuko tayari kukupa hitaji lako unalomuomba, ni wewe
ambaye unachelewa kujua mapenzi yake ili uweze kupata haja za moyo wako.
No comments:
Post a Comment