Wednesday, 24 May 2017

Kuwekwa huru mbali na sheria ya dhambi



Warumi 8:1-2
“Sasa basi, hakuna hukumu ya adhabu juu yao walio katika Kristo Yesu. Kwasababu sheria ya Roho wa uzima ule ulio katika Kristo Yesu imeniacha huru mbali na sheria ya dhambi na mauti.”

Hii ni kwa namna gani?
Kipindi kile cha sheria ya Musa, watu walikuwa wanaishi kutegemea mwili na si rohoni. Mwili ni dhaifu kwa habari ya kufuata sheria za Mungu. Hii ilitokana na laana ya dhambi iliyofanyika pale katika bustani ya Edeni ambapo Eva alidanganywa na nyoka na kula tunda alilokatazwa na Mungu. Walipoondolewa kutoka bustanini, utawala wote waliokuwa nao Adam na Eva uliingia mikononi mwa shetani ambaye ni mleta laana.

Hata sheria ya Mungu iliyoletwa na Musa ilipokuja, kwasababu ya laana, watu  hawakuweza kuitimiza sheria. Watu walibaki wakiwa wanahukumiwa kwasababu ya dhambi zao na kuishi maisha ya kushindwa kila wakati.

Ashukuriwe Mungu mwenyenzi kumleta Yesu Kristo mwanane na kuja kufa kwa ajili yetu na kuondoa sheria ya dhambi na mauti iliyoletwa na shetani, na kuweka sheria ya uzima ndani ya kila atakaye muamini. Ukiamua kumwamini Kristo Yesu, basi hakutakuwa na hukumu ya dhambi na mauti juu yako kwasababu sheria ya roho wa uzima inakuweka huru mbali na sheria ya dhambi na mauti. Na hii inawezekana kwasababu wewe utakuwa hauenendi tena katika mwili ambao ni dhaifu kupokea sheria za Mungu, bali uko katika roho ambamo sheria ya Mungu inawekwa ndani yako automatically, wala hutakuwa na haja ya kutumia nguvu kuacha dhambi. Utajikuta tu unajua hii ni dhambi na hivyo utaachana nayo au utakaa mbali nayo.

Mpendwa msomaji ukiona bado unatumia nguvu sana kuacha dhambi na kwa muda mrefu, nakusihi ujichunguze kwa habari ya wokovu wako kwasababu hutakiwi kuishi na tamaa za mwili wakati unatakiwa kutawaliwa na Roho Mtakatifu ili akuweke huru mbali na dhambi na mauti.

No comments:

Post a Comment