Wednesday, 17 January 2018

Mwanzo wa Mwaka mpya


Tunanamshukuru Mungu kwa kutuingiza kwenye mwaka mwingine mpya.
Mungu analo kusudi katika maisha yako, kwani hadi leo hii amekuweka hai ukiwa katika hali hiyo uliyonayo. Maadam uko hai, unayonafasi ya kufanya kitu cha tofauti katika maisha yako. Nina maana unao uwezo wa kubadilisha hali uliyonayo sasa ukaifanya ikawa bora zaidi.

Embu tuangalie maandiko, Waefeso 2:6 inasema "Akatufufua pamoja nae, akatuketisha pamoja nae katika ulimwengu wa roho, katika Kristo Yesu...."

Hapa tunaona ya kuwa baada ya wewe kumpokea Yesu Kristo, Yesu alikufufua na kukuweka katika ulimwengu wa roho. Hili ni neno linalotia hamasa sana yakuwa kumbe wewe sasa hivi uko katika ulimwengu wa roho. Na tunajua ya kuwa ukiwa katika ulimwengu wa roho unaouweza wa kufanya chochote utakacho kwasababu unakuwa hauna ukomo (limit)

Umeshawahi kusikia hata mapepo yanaweza kufanya chochote au kuingia popote bila shida, hii ni kwasababu wako katika ulimwengu wa roho. Mungu yuko katika ulimwengu wa roho na hata shetani pia yuko katika ulimwengu wa roho.

Ndugu yangu, ukiwa katika ulimwengu wa roho, unakuwa na uweza wa kutenda mambo.

Sasa umeshajua ya kuwa Yesu alikufufua pamoja nae na amekuketisha pamoja nae katika ulimwengu wa roho. Anza kuamini uko katika ulimwengu wa roho sasa, na anza kutumia mamlaka uliyonayo kwa kupitia neno la Mungu kuamuru vitu vinavyokuzunguka, kuumiza , shindikana, kufanyika kama unavyotaka wewe.

Uwezo unao na mamlaka unayo. Jifunze zaidi maneno ya Mungu ili uweze kujua namna unavyoweza kupata ushindi wakati huu na utaona utakavyobadilisha hali yako na maisha yako kwa urahisi kabisa.
Je ni ada ya mtoto hauna? Je ni kazi hauna? Je hujapata wa kukuoa? Je una ugonjwa unaokusumbua? Je una madeni yanayo kushinda kulipa? Je una kesi mahakamani? Yote hayo yako katika uwezo uliopewa na Mungu kwa kupitia Yesu Kristo. Acha kukata tamaa, anza leo kutumia mamlaka uliyonayo.