Friday, 31 August 2018
Sunday, 4 February 2018
Maisha Ya Amani
Karibu msomaji wangu
Leo tunajifunza kuhusu AMANI.
Nini maana ya Amani. Amani ni ile hali ya kuishi bila wasiwasi au mashaka ya aina yoyote.
Amani ni hatua ya juu sana ya maisha ya mtu yenye kutamaniwa. Palipo na amani ndipo mtu anapenda kuishi hapo.
Ni namna gani mtu anaweza kuishi maisha ya Amani?
Ngoja tuone fomula ifuatayo ili kuweza kupata amani.
IMANI - HOFU = AMANI
Ndiyo, ukiwa na imani katika kitu fulani, halafu ukatoa hofu inayokuzunguka basi utakuwa na amani. Ukiifahamu hii fomula na kuifanyia kazi, itakusaidia kuvuka salama katika maeneo mengi unayoyapitia katika maisha yako.
Ukisoma Waebrania 11:1 inasema "Imani ni kuwa na hakika ya mambo yatarajiwayo, ni bayana ya mambo yasiyoonekana."
Ukiwa unaamini neno la Mungu kuhusu jambo fulani katika maisha yako, na ukiondoa hofu inayokuzungukia juu ya hilo jambo, utakuwa na Amani.
Hofu ni kule kuangalia hali inayokuzunguka na kukuogopesha. Inaweza kuwa ya wakati huohuo au ya kufikirika kwa wakati ujao.
Ili kuweza kuishi maisha ya kumpendeza Mungu, usiwe mtu wa hofu. Ondoa hofu katika kila unalolifanya. Wewe amini tu kuwa unaweza au inawezekana kupona ugonjwa huo, kupata kazi nzuri, kupata ndoa nzuri, kupata watoto wema, kuwa mtu muhimu n.k. Hii ndiyo imani.
Usiangalie ni hali gani unayoipitia kwa sasa, bali macho yako yaone kile unachokiamini na ndipo utapata Amani na pole pole utaanza kuona kile kitu unachoamini kinatokea.
Mara zote hofu ndiyo inayokufanya usipige hatua, na unakuwa sikuzote mtu wa sintofahamu. Yaani sijui itakuwaje katika kila jambo. Ukiona hali hiyo ujue uko katika hofu.
Amua leo kuondoa hofu katika maisha yako na uamini kile alichosema Mungu kuwa utaweza na utapata. Hapo utaanza kuona maisha yako yanabadilika na kuwa ya Amani.
Leo tunajifunza kuhusu AMANI.
Nini maana ya Amani. Amani ni ile hali ya kuishi bila wasiwasi au mashaka ya aina yoyote.
Amani ni hatua ya juu sana ya maisha ya mtu yenye kutamaniwa. Palipo na amani ndipo mtu anapenda kuishi hapo.
Ni namna gani mtu anaweza kuishi maisha ya Amani?
Ngoja tuone fomula ifuatayo ili kuweza kupata amani.
IMANI - HOFU = AMANI
Ndiyo, ukiwa na imani katika kitu fulani, halafu ukatoa hofu inayokuzunguka basi utakuwa na amani. Ukiifahamu hii fomula na kuifanyia kazi, itakusaidia kuvuka salama katika maeneo mengi unayoyapitia katika maisha yako.
Ukisoma Waebrania 11:1 inasema "Imani ni kuwa na hakika ya mambo yatarajiwayo, ni bayana ya mambo yasiyoonekana."
Ukiwa unaamini neno la Mungu kuhusu jambo fulani katika maisha yako, na ukiondoa hofu inayokuzungukia juu ya hilo jambo, utakuwa na Amani.
Hofu ni kule kuangalia hali inayokuzunguka na kukuogopesha. Inaweza kuwa ya wakati huohuo au ya kufikirika kwa wakati ujao.
Ili kuweza kuishi maisha ya kumpendeza Mungu, usiwe mtu wa hofu. Ondoa hofu katika kila unalolifanya. Wewe amini tu kuwa unaweza au inawezekana kupona ugonjwa huo, kupata kazi nzuri, kupata ndoa nzuri, kupata watoto wema, kuwa mtu muhimu n.k. Hii ndiyo imani.
Usiangalie ni hali gani unayoipitia kwa sasa, bali macho yako yaone kile unachokiamini na ndipo utapata Amani na pole pole utaanza kuona kile kitu unachoamini kinatokea.
Mara zote hofu ndiyo inayokufanya usipige hatua, na unakuwa sikuzote mtu wa sintofahamu. Yaani sijui itakuwaje katika kila jambo. Ukiona hali hiyo ujue uko katika hofu.
Amua leo kuondoa hofu katika maisha yako na uamini kile alichosema Mungu kuwa utaweza na utapata. Hapo utaanza kuona maisha yako yanabadilika na kuwa ya Amani.
Wednesday, 17 January 2018
Mwanzo wa Mwaka mpya
Tunanamshukuru Mungu kwa kutuingiza kwenye mwaka mwingine mpya.
Mungu analo kusudi katika maisha yako, kwani hadi leo hii amekuweka hai ukiwa katika hali hiyo uliyonayo. Maadam uko hai, unayonafasi ya kufanya kitu cha tofauti katika maisha yako. Nina maana unao uwezo wa kubadilisha hali uliyonayo sasa ukaifanya ikawa bora zaidi.
Embu tuangalie maandiko, Waefeso 2:6 inasema "Akatufufua pamoja nae, akatuketisha pamoja nae katika ulimwengu wa roho, katika Kristo Yesu...."
Hapa tunaona ya kuwa baada ya wewe kumpokea Yesu Kristo, Yesu alikufufua na kukuweka katika ulimwengu wa roho. Hili ni neno linalotia hamasa sana yakuwa kumbe wewe sasa hivi uko katika ulimwengu wa roho. Na tunajua ya kuwa ukiwa katika ulimwengu wa roho unaouweza wa kufanya chochote utakacho kwasababu unakuwa hauna ukomo (limit)
Umeshawahi kusikia hata mapepo yanaweza kufanya chochote au kuingia popote bila shida, hii ni kwasababu wako katika ulimwengu wa roho. Mungu yuko katika ulimwengu wa roho na hata shetani pia yuko katika ulimwengu wa roho.
Ndugu yangu, ukiwa katika ulimwengu wa roho, unakuwa na uweza wa kutenda mambo.
Sasa umeshajua ya kuwa Yesu alikufufua pamoja nae na amekuketisha pamoja nae katika ulimwengu wa roho. Anza kuamini uko katika ulimwengu wa roho sasa, na anza kutumia mamlaka uliyonayo kwa kupitia neno la Mungu kuamuru vitu vinavyokuzunguka, kuumiza , shindikana, kufanyika kama unavyotaka wewe.
Uwezo unao na mamlaka unayo. Jifunze zaidi maneno ya Mungu ili uweze kujua namna unavyoweza kupata ushindi wakati huu na utaona utakavyobadilisha hali yako na maisha yako kwa urahisi kabisa.
Je ni ada ya mtoto hauna? Je ni kazi hauna? Je hujapata wa kukuoa? Je una ugonjwa unaokusumbua? Je una madeni yanayo kushinda kulipa? Je una kesi mahakamani? Yote hayo yako katika uwezo uliopewa na Mungu kwa kupitia Yesu Kristo. Acha kukata tamaa, anza leo kutumia mamlaka uliyonayo.
Subscribe to:
Posts (Atom)
-
Zaburi 107:19-20 inasema “Wakamlilia Bwana katika shida zao. Akawaponya na shida zao.Hulituma neno lake huwaponya. Huwatoa katika maang...
-
Msongo wa mawazo yaani stress hutokea pale ambapo mwili unapotoa homoni za kuweza kupigana na hiyo hali ya msongo wa mawazo. Hiyo hali ikiwa...
-
Luka 12: 32-34 "Msiogope enyi kundi dogo, maana Baba yenu amependa kuwapeni ufalme. Uzeni mali yenu mkawape maskini hizo fedha. Jifa...